Othman Masoud Othman
@othmasoud
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Taifa
ID:1366696384787791875
02-03-2021 10:26:35
258 Tweets
10,5K Followers
39 Following
Leo Aprili 24, 2024 nimepata fursa ya kukutana na kufanya Mazungumzo na Mshauri wa Mambo ya Kisiasa kutoka Ubalozi wa Uingereza Nchini Tanzania,UK in Tanzania , Bw. Samuel Raff, aliyefika kujitambulisha Ofisini kwangu Migombani Mjini Unguja.
Nimefarijika sana kuhudhuria na kupata fursa ya kubadilishana mawazo na vijana wa chama chetu cha ACTWazalendo, katika Kongamano Maalum la Ngome ya Vijana, hakika mahudhurio yao ni Ujumbe tosha kwamba wapo tayari na Mabadiliko, Zanzibar Mpya, Zanzibar Moja Mamlaka Kamili.
Leo Aprili 17, 2024 nimepata fursa ya kukutana na kuzungumza na Viongozi mbali mbali, wa chama chetu cha ACTWazalendo katika Kikao cha Pamoja cha Wajumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu, waliopo kisiwani Unguja, kikao kilichofanyika katika ofisi zetu Vuga Wilaya ya Mjini Unguja
Ahsanteni sana, Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama chetu cha ACTWazalendo na Wanachama wenzangu wote kwa ujumla, kwakuendelea kuniamini, Naahidi kwenu kuidumisha Imani hii tena kwa mapenzi makubwa.
Ahsanteni sana Wanachama na Viongozi wa Chama chetu cha ACTWazalendo
#TaifalaWote #MaslahiYaWote
#ZanzibarMpya #ZanzibarMoja
#MamlakaKamili
#MiminaZanzibar #ZanzibarnaMimi
Leo Februari 24, 2024 nimerejesha Fomu ya Kugombea Nafasi ya Uwenyekiti wa Chama chetu cha ACTWazalendo Taifa, huko katika Ofisi zetu za Chama Vuga Mjini Unguja, Ahsanteni sana Wanachama na Viongozi wenzangu kwakujumuika nami katika hili. #SOTENIWASHINDI
Februari 12, 2024, nilipata fursa ya kujumuika pamoja na Viongozi Wakuu wa Chama chetu cha ACTWazalendo, katika Kikao cha Halmashauri Kuu kilichofanyika huko katika Ofisi ya Makao Makuu ya Chama Magomeni Mikumi, Jijini, Dar es salaam.
Leo Januari 27, 2024 nimepata fursa ya kuungana na Viongozi na Wananchi mbali mbali, tukiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu, katika Zoezi la Upandaji Miti, huko Donge Muwanda, Mkoa wa Kaskazini Unguja
Leo Januari 27, 2024 nimepata fursa ya kuungana na Viongozi na Wananchi mbali mbali, tukiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu, katika Zoezi la Upandaji Miti, huko Donge Muwanda, Mkoa wa Kaskazini Unguja.