Ezra 10: 4 (SUV)
4 Inuka; maana shughuli hii yakuhusu wewe; na sisi tu pamoja nawe; uwe na moyo mkuu, ukaitende.
#Nenolasiku
#NENOLASIKU
Zaburi 105:4 BHN
Tafuteni msaada kwa Mwenyezi-Mungu mwenye nguvu; mwendeeni Mwenyezi-Mungu daima.
#NenoLaSiku
Yesu akamjibu, “Ninakwambia hakika, mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona Ufalme wa Mungu.”
Yohana 3:3
#NENOLASIKU
Nehemia 8:10
Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa Bwana wetu; wala msihuzunike; kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu.
#NenoLaSiku
Tazama jinsi ulivyo mkuu wema wako, uliowawekea akiba wakuchao, ambao huwapa wale wakukimbiliao machoni pa watu.
Zaburi 31:19 NEN
#NenoLaSiku
Lakini mlango ni mwembamba na njia ni finyu ielekeayo kwenye uzima, nao ni wachache tu waionao.
Mathayo 7:14 NEN
2 Wakorintho 6:4 (SUV)
4 bali katika kila neno tujipatie sifa njema, kama watumishi wa Mungu; katika saburi nyingi, katika dhiki, katika misiba, katika shida;
#Nenolasiku
#NENOLASIKU
Zaburi 139:23-24
Ee Mungu, nichunguze, uujue moyo wangu,
nijaribu na ujue mawazo yangu. 24.Uone kama kuna njia iletayo machukizo ndani yangu,
uniongoze katika njia ya milele.